kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Wednesday 29 May 2013

MTANZANIA FEZA AZIDI KUNGA'ARA BIG BROTHER AFRICA....AUKWAA UKUU WA KAYA

Tunaenda vizuri, bahati inaonekana kutuangukia watanzania kwani mshiriki Feza jana ameukwaa ukuu wa kaya ama kwa lugha ya ki-big brother ‘Head of House’.

Ilikuwaje?

Baba mwenye nyumba, biggie, alitoa task ambayo washiriki walitakiwa kuelekea bustanini na kuchagua box, ambaye angechukua box la ushindi ndo huyo angekuwa mkuu wa kaya. Kama zali, bahati hiyo ilimuangika mrembo Feza. Washiriki wenzie akiwemo mtanzania Nando, walimkumbatia kwa furaha kama ishara ya kumpongeza.

Iko hivi, ukichaguliwa kuwa mkuu wa kaya, unauwezo wa kumuokoa mtu ambaye anakuwa amependekezwa atoke katika wiki hiyo. Usipofanya hivyo basi wewe mwenyewe unawekwa kikaangoni.

Feza alitumia nafasi hiyo kumuokoa Elikem ambaye ni mshiriki kutoka Ghana na kumuweka kikaangoni Betty kutoka Ethiopia. Hiyo ni siri ambayo Feza inabidi aitunze hadi siku ya Jumapili wakati wa Eviction.

Hii issue ya kumuokoa Elikem wa Ghana, je ni dalili ya shemeji shemeji mbona wazima taa? Endelea kufuatilia..

PICHA YA HOSPITALI(Helen Joseph),Ulipohifadhiwa Mwili wa Marehemu albert Mangwea



Ngwea amefariki dunia jana asubuhi katika moja ya vitongoji vya jiji la Johannesburg na baadaye wenzake walimkimbiza katika Hospitali ya St Helen Joseph.

RIBERY ALALA KITANDA KIMOJA NA KOMBE LA ULAYA PAMOJA NA MKEWE


Winga wa Bayern Munich Franck Ribery amefichua kwamba alilichukua kombe la ubingwa wa ulaya na kwenda kulala kufuatiwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Borrusia Dortmund.

Mabingwa wa Bundesliga wamefika kwenye fainali ya Champions League mara tatu katika mika minne lakini wameshinda ubingwa wa ulaya kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2001.


Na Ribery akazungumzia namna alivyosherehekea ubingwa huo mara baada ya mchezo: "Nilikuwa macho mpaka saa 11 au 12 asubuhi,"  Sky Sports News.

"Nilienda kulala kabla ya saa 12 na nikachukua kombe la ulaya nikaenda nalo kulala kwenye kitanda kimoja pamoja na mke wangu."

HII NDIO SABABU INAYODAIWA KUSABABISHA KIFO CHA NGWAIR. SOMA HAPA

ripoti kamili
Taarifa Nilizo Pata Kutoka South
Africa Kutoka Kwa Hussein
Original Ambaye Yupo Pretoria
Amesema Ngwear Amefariki Leo

Asubuhi. Alikuwa Ghetto Moja Na
Msanii M To The P.
Walivyokwenda Kuwagongea
Asubuhi Walikuta Ngwear
Amefariki Na M To The P
Amepoteza Fahamu Kabisa. Pia
Daktari Ameshatoa Taarifa Kwa
Watu Wa Karibu Wa Ngwear
Huko South Africa. Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.mtu wa karibu anasema walitakiwa kurudi dar leo lakini waliwakuta wamezima kwenye room wote wawili baada ya kuji overdose madawa ya kulevya na M to the P yupo hoi hospitali

KUTOKA KWA ROMARIO MPAKA RONALDINHO - JE NEYMAR ATAFUATA NYAYO ZA WABRAZIL WENZIE NA KUTAMBA CAMP NOU

Romário (1993), Ronaldo (1996), Rivaldo (1997), Ronaldinho (2003) na Neymar (2013). Neymar anajiunga ma urithi mzuri wa washambuliaji wa Brazil unaoundwa na wanaume wanne waliopata mafanikio makubwa katika miongo kadhaa iliyopita na kupata mafanikio makubwa ndani ya Nou Camp - sasa ni zamu  Neymar da Silva.

Romário na Ronaldo
Romário aliigusa mioyo ya mashabiki wa Barca kwenye msimu wa 1993-4, wakati alipopewa jina la “cartoon footballer” kutokana na kuwa uwezo mkubwa mno wa kucheza soka. Aliposajiliwa alihaidi kufunga mabao 30 ya ligi na akatimiza ahadi yake huku kikosi cha Cruyff kikishinda ubingwa msimu huo, Romario alirudi Brazil baada ya nusu ya msimu uliofuatia.

Mara baada ya Romario kuondoka kinda la miaka 19 - Ronaldo De Lima aliwasili Camp Nou. Alikuwa na nguvu, mwenye ujuzi na mwenye uchu wa mabao - kwenye msimu wake wa kwanza alifunga mabao 47 kwenye mechi 51.

Rivaldo na Ronaldinho
Wakati Ronaldo alipohamia Inter, Rivaldo akaja Camp Nou akitokea Deportivo. Rivaldo akawa nyota wa kikosi cha Van Gaal kilichoshinda ligi mara mbili. Alifanikiwa kushinda mchezaji wa dunia mwaka 1999.

Kuwasili kwa Ronaldinho mwaka 2003 kukaleta mageuzi makubwa kwa klabu ya Catalunya na kuleta tabasamu lilopotea na mashabiki wa Barca. Baada ya ukame wa miaka mitano bila kombe, aliiongoza Barca kushinda ubingwa wao wa pili wa ulaya jijini Paris na kushinda uchezaji bora wa ulaya na dunia kwa mara kadhaa. 

Evaristo, Giovanni and Anderson
Romário, Ronaldo, Ronaldinho na Rivaldo wanaweza kuwa ndio washambuliaji wa kibrazil waliopata mafanikio makubwa zaidi, lakini hawakuwa wabrazil pekee walioleta sura za furaha Camp Nou. Kwa mfano miaka ya1950s, Evaristo de Macedo alifunga mabao 173 kwenye 219. Miongo kadhaa baadae mwishoni mwa miaka ya 90, Giovanni Silva na Sony Anderson pia walileta sura za furaha Catalunya kwa viwango vyao.

Sasa ni zamu ya Neymar - je atafuata nyayo za magwiji ya Brazil waliomtangulia kucheza Camp Nou na kuwafunika kabisa kimafanikio? Muda utaongea.

E-Newz, 28 May 2013 ( WAKIZINGUMZIA KIFO CHA MANGWEAR )

DIAMOND AFANYA KUFURU TEMEKE, WATU WAZUNGUKA GARI LAKE ASINDIKIZWA NA GARI LA POLISI

Monday 27 May 2013

PICHA YA LEO


FEZA KESSY NA NANDO WAIWAKILISHA TANZANIA NDANI YA BBA 2013




Big Brother Africa  2013 "The Chase" imeanza kwa kasi usiku wa jana (26 may) na msanii Feza Kessy na Nando ndio wanaoiwakilisha Tanzania. kwa mujibhu wa story yake mwenyewe Nando ni mtanzania anaeishi marekani lakini ilimbidi aombe hela kwa marafiki zake kwa ajili ya kupata ticket ya kuja Tanzania kufanya usahili wa BBA, amesema kama angekosa nafasi ya kuiwakilisha Tanzania asinge juta maana pia alikua hajamuona bibi yake kwa miaka mingi, kwahiyo angekuwa kaitumia nafasi hiyo kuja kumuona bibi yake.

TAIFA STARS NDANI YA SUTI MPYA ZILIZOANDALIWA KWA AJILI YAO NA MBUNIFU SHERIA NGOWI

Wachezaji wa Taifa Stars na benchi la ufundi katika picha ya pamoja wakionesha suti zao.

Wachezaji wa Taifa Stars, benchi la ufundi na maofisa wakuu wa TBL katika picha ya pamoja wakati wa kuonesha suti mpya

Wachezaji wakifurahia huku wakishangiliwa baada ya kuonesha suti zao mpya.

John Bocco na Erasto Nyoni

Wageni waalikwa wakifuatilia matukio wakati wa hafla ya Kilimanjaro Premium Lager kukabidhi suti mpya kwa Taifa Stars.

TAIFA STARS WAONDOKA KWENDA KUIWEKEA KAMBI MOROCCO ADDIS ABABA

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka leo (Mei 26 mwaka huu) usiku kwenda Addis Ababa, Ethiopia ambapo itaweka kambi na kucheza mechi moja ya kirafiki kabla ya kwenda Morocco.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itaondoka saa 5 usiku kwa ndege ya EgyptAir ikiwa na kikosi cha wachezaji 21 chini ya nahodha wake kipa Juma Kaseja.
Timu hiyo ikiwa Ethiopia, Juni 2 mwaka huu itacheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan ambapo siku inayofuata itaondoka kwenda Marrakech, Morocco kwa kupitia Cairo, Misri. Mechi hiyo ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech.
Mbali ya nahodha Kaseja, wachezaji wengine wanaoondoka katika kikosi hicho ambacho kina wiki sasa tangu kingie kambini jijini Dar es Salaam ni Mwadini Ally na Ally Mustafa ambao wote ni makipa.
Wengine ni Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Aggrey Morris, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd na Haruni Chanongo.
Wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wako na timu yao ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo watajiunga moja kwa moja na Stars jijini Marrakech, Juni 4 mwaka huu wakitokea Maputo, Msumbiji mara baada ya mechi yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Liga Muculumana ya huko.
Katika msafara huo wa Ethiopia benchi la ufundi la Stars linaundwa na Kim Poulsen (Kocha Mkuu), Sylvester Marsh (Kocha Msaidizi),Juma Pondamali (Kocha wa makipa), Leopold Tasso (Meneja wa timu), Dk. Mwanandi Mwankemwa (Daktari), Frank Mhonda (Mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (Mtunza vifaa).

DJ NOBLE:NEW BONGO HOT MIXING 2013

 
UNAWEZA KUMCHEKI THROUGH:
Phone no:0717791274
Bbm pin:21A8EA87
Email:Yusuphjuma54@yahoo.com
Facebook:Dj noble


BREAKING NEWS: NEYMAR ATHIBITISHA ANAJIUNGA NA BARCELONA

BARCELONA wamefanikiwa kushinda mbio za kumsaini nyota wa Brazil Neymar kwa ada ya uhamisho ya  £20million kwa mkataba wa miaka mitano.

Mshambuliaji huyo sasa anaelekea barani ulaya baada ya Santos kukubali kumuuza nyota wao waliomng'ang'ania kwa miaka mingi.
Akiandika kwenyepage yake ya Instagram, Neymar alisema: "Nimeongea na marafiki na familia. Jumatatu nitajiunga na Barcelona."
Mabosi wa Barca walienda Sao Paolo kwa mazungumzo mazito kuhusu usajili wa mbrazili huyo, na wakafanikiwa kuwashawishi Santos kumuuza Neymar ambaye angeweza kuondoka bure mwezi Julai.

Neymar alitaka muda kufikiria ofa nyingine kutoka kwa wapinzani wa Barca Real Madrid lakini mwishoni akaamua kwenda Nou Camp.

Kwa usajili huu sasa Neymar atacheza atajiunga na star wa Argentina Lionel Messi na kuunda safu ya ushambuliaji inayotisha barani ulaya.

Neymar ameifungia Santos mabao 138 kwenye mechi 229 tangu mwaka 2009.

DIAMOND - LIVE PERFOMANCE IN BURUNDI

VIDEO: NEY NA DIAMOND NDANI YA DAR LIVE WIKI ILIYOPITA HIVI NDIVYO ILIVYOKUA

Saturday 25 May 2013

HUU NDIO UCHAMBUZI NA UTABIRI WANGU WA FAINALI YA BORRUSIA DORTMUND VS BAYERN MUNICH

FC Bayern wanakutana na mtihani mgumu usiku wa leo watakapocheza dhidi ya Borussia Dortmund kwenye dimba la Wembley jijini London. Leo ni siku ya kuondokana na mkosi mkubwa unaowatawala mabavarians ambao ndio timu inayoongoza kwa kufungwa kwenye UEFA Champiosn League - leo ni siku ya kufuta machungu kwa kupoteza mechi ya fainali ya mwaka jana ambayo walistahili kushinda ingawa bahati haikuwa upande wao.
Hii ni fainali ya kwanza ya wajerumani ambao wanastahili kuwemo kwenye fainali hiyo. Utakuwa mchezo mzuri wa kukumbukwa.

Dortmund, klabu inayoibuka kuwa na nguvu barani ulaya

Majeruhi: Mario Götze
Baada ya kusemwa kuwa kutolewa kawenye hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa ulaya msimu wa 2011-12, Dortmund hatimaye wameyachukulia uamakini mashindano haya kwa gaharama ya kupoteza ubingwa wa nyumbani.
Ingawa, mchezo wao kwenye Champions League umekuwa wa aina yake. Nguvu, ushirikiano, mbinu za mchezo wao zimekuwa nzuri kiasi cha kuvishinda vilabu kama Real Madrid.
Mario Götze, kiungo mchezashaji wao, ataukosa mchezo huo kutokana na majeruhi ya misuli. Alijaribu kurudisha fitness yake kupitia mazoezi, lakini bahati haikuwa yake na akaawambia mchezo wake wa mwisho wa msimu huu ulikuwa pale Santiago Bernabeu. Ujuzi ambao BVB wataukosa ni pasi muhimu, kukimbiza mpira na mashuti yenye madhara
Wachezaji wa kuchungwa.
Kukosekana kwa Gotze kutamuacha mchezashaji Marco Reus. Kiungo huyo mshambuliaji anaweza kufanya runs za hatari pia kupiga mashuti na kutoa pasi za mwisho za hatari. Kazi ya kumzuia Reus kwa hakika atapewa kiungo mkabaji wa Bayern Javi Martinez ambaye aliweza kuwazima Iniesta na Andrea Pirlo kwenye mechi za raundi zilizopita.
Robert Lewandowski amegeuka kuwa mshambuliaji wa kiwango cha dunia, ameonyesha utulivu mbele ya lango la adui ambao washambuliaji wanakosa. Ana control nzuri ya mpira, anapiga mashuti yenye kulenga goli.
Muhimu zaidi, ni hazina ya Dortmund kwenye kulinda lango - golikipa Roman Weidenfeller. Uwezo wake wa kudaka uliinyima Bayern ushindi kwenye michezo kadhaa iliyopita msimu huu.
 Beki wa kati Mats Hummels anaweza akacheza mechi ya fainali pamoja na kuwa na majeruhi. Kitu cha kuvutia kuhusu yeye ni kwamba pamoja na mlinzi kwa ujumla, lakini pia anaweza akaigharimu timu yake kwa makosa ya kizembe.
Ilkay Gündogan ni kiungo mzuri mkabaji ambaye anaweza kufanya dribbling vizuri kuwapita mabeki wa Bayern, lakini sio mzuri kwa mipira ya juu ambao ndio silaha inayohitajika kuweza kuisimamisha Bayern.
Wakati uzuri wa Dortmund inacheza vizuri hata bila kuwa na mpira, mchezo mzuri wa kupasiana unaweza ukawadhuru kwenye nusu yao ya uwanja. Pia wana udhaifu mkubwa kwenye mipira mirefu.

Bayern, wanapaa kwenye muda muafaka

Majeruhi: Badstuber, Kroos.
 Huu ni mchezo unaomaanisha kila kitu kwa Bayern, ambayo ipo kwenye kiwango cha juu kwenye muda sahihi.
The bavarians wapo kwenye moto safari hii kwenye ulinzi na ushambuliaji. Udhaifu wao uliowagharimu msimu uliopita ni nguvu ya akili, udhaifu ambao umeshashughulikiwa. Sasa hivi wana ile hali ya winning mentallity - angalia namna walivyotoka nyuma na kuwafunga Borrusia Monchengladbach 4-3.
Franck Ribéry yupo kwenye kiwango cha dunia akicheza winga ya kushoto, unaweza ukasema hivyo pia kwa Thomas Muller ambaye anashughulika na majukumu ya kushambulia aliyokuwa nayo Toni Kroos.
Bastian Schweinsteiger na kila kitu cha kutoa kwenye mchezo huu. Ni package iliyokamilika kama mchezaji, box to box midle, yupo kwenye kiwango cha juu sana.
Uzuri wa Bayern hivi sasa mpaka wachezaji ambao walikuwa wavivu kama Arjen Robben wanakaba, timu yote inakaba kwa pamoja na wanashambulia kwa pamoja.

MBINU

Mtu yoyote ambaye angeniuliza timu gani yenye mbinu kali kati ya BVB na Real Madrid: jibu lingekuwa Dortmund. Sio tu kwamba wanaijua vizuri Bayern Munich, bali pia ni hatari sana kwenye mchezo wa kushambulia. Ubora wa umewaumiza wapinzaani wengi, lakini staili yao inayofanana na Barca ndio ambayo Bayern wanaiweza kwenye kucheza dhidi nayo.
Dortmund watahitaji kucheza mchezo wa kupelekea mashambulizi mbele, kupitia katikati ya uwanja kwa sababu ndio mchezo wanaouweza zaidi - wakipeleka mipira kwa Robert Lewandoski.
Kwa upande wa Bayern, mshambuliaji Mario Mandzukic (au Mario Gomez) wataungana na mchezeshaji Thomas Müller kuzuia mistari ya pasi kwenye kiungo kwa presha huku wakirudi nyuma taratibu
Hii itaaminisha Dortmund itabidi watumie zaidi winga kwenda mbele. Hivyo ikiwa BVB watapeleka mpira upande wa kushoto Arjen Robben na Javi Martinez wata press upande huo kuzia mashambulizi. Ikiwa watapeleka upande wa kushoto Frank Ribery na Bastian Schweinsteiger watazuia upande huo. Hii itawasaidia Lahm na Alaba kupambana akina Reus.
Hili linaweza kuwalazimisha BVB kutumia mipira ya juu ambayo Bayern wanaimudu pia, hivyo kuwafanya Dortmund kuwa na option moja tu kucheza sana mpira kwenye nusu yao ya uwanja na kujaribu kufanya counter. Hivyo nafasi zao za kufunga zitakuwa pungufu - au italawazimu wachezaji wa Dortmund kuwashinda wa Bayern kwenye vita ya one-on-one au kunufaika na makosa ya wachezaji wa Bayern kama ilivyokuwa kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Monchengladbach wiki iliyopita. Lakini pia Bayrn wanaweza wakawa wamepata funzo kupitia mchezo huo na kutoruhusu makosa yale yasijirudie dhidi ya Borrusia Dortmund usiku wa leo pale Wembley.
Ikiwa Bayern watacheza kwenye kiwango cha juu usiku wa leo basi itawachukua BVB kutumia vipaji binafsi zaidi vya wachezaji kuweza kushinda.
 
Vita binafsi leo hii itakuwa kati ya winga wa kushoto wa Bayern Frank Ribery vs Lukasz Piszczek. Kwa spidi aliyonayo Mpoland huyo, na uwezo wake wa kuzuia itamchukua uwezo mwingi sana Frank Ribery kuweza kupita.
Mara ya mwisho Bayern wameifunga Dortmund, walimtumia zaidi Toni Kroos na uwezo wake wa kumiliki mpira - Muller hana uwezo mkubwa wa kukaa na mpira kama ilivyo kwa Kroos hivyo mambo yanaweza magumu kiasi.

Utabiri wangu nawapa Bayern nafasi ya kushinda. Mafunzo waliyoyapata miaka iliyopita hasa msimu uliopita dhidi ya Chelsea yatawapa hali ya kupigana zaidi. Hata kama wataanza kufungwa, watashindana na kuhakikisha safari hii wanaepukana na mkosi wa fainali ya Champions League. Dortmund wana mtindo wa kupaniki - angalia katika mechi ya pili dhidi ya Madrid nusura waondolewe pamoja kuwa walikuwa na hazina ya mabao 4-0.

Vikosi vinavyoweza kuanza

FC Bayern (4-2-3-1) Neuer – Lahm, Boateng, Dante, Alaba – Martinez, Schweinsteiger – Robben, Müller, Ribéry – Mandzukic
Borussia Dortmund (4-2-3-1) Weidenfeller – Piszczek, Subotic, Hummels, Schmelzer – Gündogan, Kehl – Blaszczykowski, Reus, Grosskreutz – Lewandowski
Location: Wembley Stadium, London
Referee: Nicola Rizzoli (Italy)

MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS MOROCCO


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).
Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.
Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.
Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni   Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
Mei 25                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni     Uwanja wa Karume
Mei 26                 Saa 3 asubuhi                            Uwanja wa Karume

AMRI KIEMBA ASAINI YANGA

WAKATI Haruna Niyonziam akiwa amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga, habari zilizotufikia hivi punde zinasema kiungo wa Simba, Amri Kiemba amesajiliwa na Yanga tayari kwa kuitumikia timu hiyo kwa msimu ujao.
Akizungumza na mtandao huu, mtu mmoja kutoka kamati ya usajili ya Yanga, amesema Kiemba amesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili ili kuongoza nguvu katika safu ya usajili ya Yanga.
Mtandao huu unaahidi kuwasiliana na Kiemba muda mfupi atakapotoka mazoezini katika kambi ya Taifa Stars kujiandaa na mechi ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2014.
Atakapotoka mazoezini mtandao huu utawasiliana naye kiungo huyo ili aweze kueleza ukweli juu ya usajili wake kwa Yanga.
Kiemba aliwahi kuichezea Yanga miaka ya nyuma kabla ya kutimka katika timu hiyo.

BREAKING NEWS: RAMA MLA WATU AACHIWA HURU




Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imeamua kumuachia huru Ramadhani Selemani Mussa ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya kukutwa na kichwa cha mtu. Rama, ambaye muda wote huo alikuwa rumande gereza la Segerea akisota kusubiri hukumu yake, alikamatwa hospitali ya Muhimbili mwaka 2008 ambapo pia alikiri kuwa alikuwa na tabia ya kula nyama za watu ambayo amefundishwa kichawi toka alipokuwa mdogo. Mahakama imemuachia huru kwasababu mtuhumiwa alitenda kosa hilo pasipo kuwa na akili timamu. Hata hivyo mahakama hiyo imetoa agizo la kuendelea kumuweka kijana huyo katika hospitali ya wagonjwa wenye matatizo ya akili, hospitali ya Isanga iliyopo Dodoma mpaka pale atakapona ndipo aruhusiwe kurudi mtaaani.habari kutoka karibu ndani

KANYE WEST AFUNGUKA RASMI....ATEGEMEA KUWA BABA HIVI KARIBUNI.....

BIG BROTHER AFRICA(THE CHASE) NDANI YA KING'AMUZI CHAKO J2 HII

DIAMOND,NEY WA MITEGO BAADA YA KUANGUSHA SHOO YA KIJANJA DAR LIVE HAWA HAPA TENA MAISHA CLUB J2 HII

THIS IS DIAMOND-IN CONGO

Wednesday 22 May 2013

ATTENTION new Audio song MRAP FEAT DEDDY


produced by Pancho Latino na Hammy B kutoka B Hits, ni single mpya kutoka kwa Rapper mdogo Tanzania M Rap feat Deddy. isikilize hapo chini 

Tz All Female Stars - Kidole Kimoja(FESTULA Official Video)

Amour Genius --- Bongo Movie (Official Video)

OFFICIAL VIDEO(2013)Witnesz ft Ochu Sheggy_zaga zaga

OFFICIAL VIDEO Juma Nature FT Tundaman_Haipotei

WASANII WANAODAIWA KUJIUNGA NA CHADEMA 2013


mh.Joseph mbilinyi akiwa na msanii wa hip hop prof jay

K wa mapacha akiwa na Mbunge wa Ubungo Mh.john mnyika

PICHA YA SIKU

PICHA ZA WAREMBO WA REDD'S MISS KIGAMBONI 2013


Warembo wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Kigamboni wakiwa kwenye mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na kinyang'anyiro hicho kitakachofanyika Ijumaa Juni 7 mwaka huu kwenye ukumbi wa Navy Beach ulioko Kigamboni.

CPwaa ateuliwa kuwa msimamizi mkuu na MC wa michuano ya Foosball

Msanii maarufu wa kimataifa wa muziki wa kizazi kipya CPwaa ateuliwa na kampuni ya bia Heineken Tanzania kusimamia michuano ya mpira wa mezani (Foosball) pamoja na kutangaza na kuhamasisha mchezo huo wakati wa mashindano ambayo ni endelevu.Mpango huo ulikamilishwa kati ya kampuni ya Brainstormmusic & Media Co. Ltd na Heineken Tanzania Limited

Sharon Mariwa Meneja Muenezi Biashara Brainstormusic, Caroline Kakwezi, Meneja Masoko wa Heineken Tanzania, Uche Unigwe – Mkurugenzi Mkuu wa Heineken Tanzania, kulia Cpwaa na Ronald Louis Meneja Opereshini wa Brainstormusic.

Sharon Mariwa Meneja Muenezi Biashara Brainstormusic, Caroline Kakwezi, Meneja Masoko wa Heineken Tanzania na Uche Unigwe – Mkurugenzi Mkuu na Cpwaa msanii maarufu wakishikana mikono na Mkurugenzi wa Heineken Tanzania baada ya kusaini mkataba wa kuteuliwa kuwa msimamizi na MC wa michuano ya mpira wa mezani (Foosball) kulia ni Ronald Louis Meneja Opereshini wa Brainstormusic.

KAGAME CUP: SIMBA KUNDI MOJA NA APR, YANGA DHIDI YA VITAL O NA EXPRESS FC



CECAFA 2013
GROUP A; Merriekh El Fasher (Sudan), Simba (TZ), Al Mann (Somalia) & APR (Rwanda).
GROUP B; Hilal Kadougli (Sudan), Ahli Shandi (Sudan), Al Nasr (S.Sudan), Tusker (Kenya) & Super Falcon (Zanzibar)
GROUP C; Yanga (Tanzania), Express FC (Uganda), Vitalo (Burundi) & AS Port (Djibouti).

Tuesday 21 May 2013

OFFICIAL VIDEO: CAMP MULLA FT WONDA BOY "OH MA GAD"

NGASA ATAMBULISHWA RASMI YANGA angalia PICHA

Mrisho Ngasa akiongea na waandishi wa Habari jana makao makuu ya klabu ya Yanga baada y akutambulishwa rasmi jana tar 20/05/2013

Picha Mbalimbali za Show ya "Usiku wa Kumtoa Mama Yeyoo Nje ya Box" Ndani ya Maisha Club

Weusi jana walipiga show iliyopewa jina la "Usiku wa kumtoa mama Yeyoo Nje Box" kwenye ukumbi wa New maisha  club jijini Dar es Salaam,G nako,Nikki wa pili,Joh Makini,Lord Eyez,Peter Msechu, Ben pol walikuwa ni miongoni mwa waliotoa burudani..









SHILOLE FT HASSAN VOCHA - PAKA LA BAR (OFFICIAL VIDEO 2013)

Sunday 19 May 2013

KIMENUKA IRINGA,MAPAMBANO KATI YA MACHINGA NA POLISI YAMWEKA PABAYA MBUGE MSIGWA SASA KUFIKISHWA MAHAKAMANI KESHO



Mbunge mchungaji  Peter Msigwa
Polisi  waliotoka  kumkamata  mbunge Msigwa  leo 





 Gari ya  mbunge Msigwa kabla ya  kukamatwa  leo kwa kuhusishwa na vurugu
MASAA  zaidi ya 6 ya mapambano kupiga  mabomu ya machozi na kurushiana  mawe kati ya wafanyabiashara  ndogo  ndogo (machinga ) na  askari  wa  kikosi cha  kutuliza  ghasia (FFU) mkoani Iringa  yaishia pabaya  kwa  jeshi la  polisi kumkamata  mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa  (chadema) na  watu  wengine zaidi ya 60


Polisi  watumia  mabom ya machozi  kutawanya machinga  wapiga mabomu hadi stendi kuu ya mabasi  abiria  walazimika  kutimua  mbinu na kuacha mizigo  yao katika magari   huku machinga  hao wakitumia mawe  na kuchoma mataili  moto barabarani  kuvunja vioo vya gari  la Zimamoto na kuharibu mali mbali mbali kama  njia ya  kupambana na  polisi
Tukio hilo la Mapambano  kati ya machinga na polisi lilitokea leo  kuanzia  muda wa saa 3  asubuhi  na kuendelea  hadi saa 8 mchana katika  eneo la Mashine  tatu  mjini  Iringa na maeneo mbali mbali ya mji  wa Iringa .

Mtandao huu wa na simonbango.blogspot.com ambao ulituma wawakilishi zake  eneo la  tukio  toka  saa 12  za asubuhi  ya jana  alishuhudia kundi kubwa la askari  wa FFU wakiwa na gari la maji ya  kuwasha ambao  wakesha wakilinda  eneo hilo .

Askari  huo  walilazimika  kukesha wakilinda eneo hilo  kufuatia  kauli ya  mbunge  Msigwa aliyoendelea  kuitoa katika  mikutano yake ya hadhara  mjini hapa  kuwhamasisha  machinga  hao ambao  Halmashauri ya Manispa ya  Iringa  iliwahamisha  eneo hilo la mashine tatu  na kuwapeleka  eneo la Mlandege kabla ya  mbunge Msigwa kuwahamasisha  kurejea  tena  eneo hilo.

Kabla ya  mbunge Msigwa  kufika  eneo hilo majira ya  saa 3 asubuhi machinga  hao ambao  walikuwa  wamejikusanya makundi madogo madogo   bila  kupanga  biadhaa zao  walisikika  wakidai  kumsubiri  mbunge Msigwa kama alivyopata  kuwaahidi  kuwa atafika  eneo hilo kuungana nao kwa  kuwa machinga  mpya  .

Hata  hivyo baada  ya mbunge  huyo kufika akiwa na gari lake  la kibunge  ambalo lilikuwa lilikokota tela  la  kuhifadhia mizigo  alisimama  eneo hilo na  kuendeleza msimamo  wake  wa kuwataka machinga  kupambana na baada ya  muda alitoweka  eneo hilo kabla ya  polisi  kuanza  kuwatawanya  machinga hao kwa mabomu ya machozi .

Wakizungumzia  hali hiyo  ambayo ni ya  kwanza kutokea katika  mji  wa Iringa wakazi  wa mji  wa Iringa  walisema  kuwa mbunge  na  viongozi  wengine  wa  serikali  wanapaswa  kulaumiwa kwa  kushindwa  kutumia njia nzuri ya  kukutana  kwa ajili ya kumaliza  mvutano huo  ambao unaendeshwa  kisiasa  zaidi.

Festo Sanga  alisema  kuwa  hali  ilipofikia  ni mbaya zaidi na  hivyo  busara  zinahitajika kwa ajili ya  kutatua  tatizo  hilo  ikiwa ni pamoja na kutazama  eneo zuri kwa ajili ya machinga  bila  kuendelea  kuonyeshana  ubabe .

Sanga  alisema  kuwa machafuko  yaliyojitokeza leo   ni machafuko ambayo wakazi  wa mji  wa Iringa  walikuwa  wakishuhudia katika  vyombo  vya habari  katika  mikoa  mingine  ukiacha  lile la Septemba 2 mwaka  jana lililotokea  kijiji  cha Nyololo kati ya  wafuasi  wa Chadema na polisi na kupelekea kifo cha aliyekuwa mwenyekiti  wa klabu  ya  waandishi  wa habari mkoa  wa Iringa marehemu Daud Mwangosi.

“Kweli katika hili  mbunge wetu hapaswi kuendelea  kulazimisha machinga  kuvunja  sheria  ila anayo nafasi ya  kukutana na viongozi  wenzake  ili  kutafuta  suluhu  ya jambo  hilo vinginevyo wanaoteseka  na machinga na  wale  waliokamatwa kwa  vurugu hizo  ujue  wengi  waliopigwa mabomu ya machozi si machinga  wengine  walikuwa  wasafiri na badhi yao  walikuwa  wakielekea makanisani ”

KUhusu  kukamatwa kwa mbunge  huyo na kuhojiwa na  polisi  juu ya vurugu  hizo Sanga  alisema kwa upande  wake analipongeza  jeshi la  polisi kwa  kutumia busara  zaidi  ya  kumkamata  mbunge   kama mhusika mkuu  na  kuliomba  jeshi la  polisi kuwaachia  wananchi  waliokamatwa  kwa  vurugu  hizo.

Huku  Sarah Kalinga  alidai  kuwa  chanazo cha machafuko hayo ni mvutano kati ya  CCM na Chadema na  kuwa  ilipaswa  vyama vyote  viwili  kukutana na  kuwasaidia  machinga  badala ya  kuwanyanyasa  kwa  kutumia nguvu  kuwabana .

Hata   hivyo  alisema wao kama walalahoi wanampongeza  mbunge wao kwa kuonyesha kuwapigania japo haungi mkono njia  inayotumiwa na mbunge ya  kuwahamasisha   kuvunja  sheria na kuwa  matatizo na majeraha  wanapata  wao  wananchi  na sio mbunge.

Awali  mbunge mchungaji Msigwa  kabla ya  kukamatawa na  jeshi la  polisi alitoweka katika mazingira  tata katika  eneo hilo la mashine  tatu na  kuibukia eneo la chuo  kikuu cha Tumaini Iringa ambako kulikuwa na harambee  ya  kuchangia Kanisa na mgeni  rasmi akiwa  waziri mkuu mstafu Frederick Sumaye na mara  baada ya  shughuli  hiyo  kumalizika ndipo alipokamatwa na polisi na kufikishwa  kituo cha  polisi.

Kabla ya  kukamatwa  kwake mbunge Msigwa alizungumza na mwandishi  wa habari hizi na kuwa  yupo tayari kukamatwa  wakati  wowote na  kuwa kamwe  ataendelea  na msimamo  wake  wa  kuwataka Machinga  kufanya  biashara  eneo hilo.

Mbali ya  kukamatwa  kwa  mbunge  Msigwa  kwa  kuhusishwa na vurugu  hizo pia  jeshi la  polisi  mkoani Iringa  linawashikilia  watu  wengine  zaidi ya 60 akiwemo  aliyekuwa kampeni meneja  wa Chadema  jimbo la Iringa mjini na mgombea  udiwani  kata ya  kwa Kilosa  Abuu Changawa Majeck.

Huku  idadi ya majeruhi  waliojeruhiwa kwa  kupigwa mawe na machinga na  badhi ya machinga  waliokamatwa kwa  vurugu  hizo pia wakijeruhiwa  vibaya  wakati  wakipambana na  polisi hao.

Taarifa  kutoka  jeshi  la polisi zilizothibitishwa na kamanda  wa polisi mkoa  wa Iringa Michael Kamuhanda  zinadai  kuwa  watu  zaidi ya 60 ndio  wamekamatwa  hadi  sasa na  jitihada za  kuwasaka wengine  waliohusika katika  vurugu  hizo ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa wa mali  za  wananchi unaendelea.

Huku akidai  mali  mbali mbali  zimeharibiwa likiwemo gari  hilo la zimamoto mjini Iringa pamoja na uharibifu  mwingine  mdogo  mdogo  wa mali za  wananchi .

Jeshi  hilo la polisi  limesema kamwe halipo tayari  kumwachia mbunge Msigwa kwa leo hadi hapo atakapofikishwa mahakamani Kesho