Denis Mtima na Irene ProfilWAKATI Oparesheni Fichua Maovu (OFM) inayoendeshwa na Global Publishers ikiwa mzigoni, imenasa tukio la fedheha kwa njemba mmoja akichezea kichapo ‘hevi’ kutoka kwa wanawake waliosadikiwa kuwa machangudoa.
Katika
tukio hilo lililojiri hivi karibuni majira ya asubuhi, maeneo ya Afrika
Sana jijini Dar, jamaa huyo alidaiwa kuopoa changu ambaye alikwenda
kumpa ‘mambo’ ya kiutu uzima kisha wakazinguana.Mashuhuda wa tukio hilo ambao kwa sehemu kubwa walikuwa ni madada poa, walidai kuwa baada ya jamaa huyo kupewa huduma ya penzi jirani na eneo hilo aligoma kulipa hivyo timbwili zito likaibuka.
Ilidaiwa
kuwa wakati jamaa huyo akitoka nduki, wanawake hao waliounda umoja wao
walipiga kelele za mwizi na kusababisha wenzao waliokuwa jirani
kufanikiwa kumdhibiti kisha kumpa kichapo huku wakimchania nguo na kuzua
taharuki kubwa.Pamoja na kufurukuta, jamaa huyo alishindwa kuhimili mangumi ya wanawake hao waliokuwa na hasira ya ajabu hadi akajikuta akitokwa na kijasho chembamba kabla ya kufanikiwa kuwakimbia.
Akizungumza
na OFM, dada huyo aliyegoma kujitambulisha alisema kwamba jamaa huyo
aligoma kutoa kiasi cha fedha walichokubaliana (aligoma kutaja) kabla ya
kwenda kufanya mapenzi.“Haiwezekani mtu tumekubaliana vizuri na amepata huduma safi, iweje agome kutoa mtonyo (fedha)? Hii ni kazi kama kazi nyingine kwa nini asiiheshimu? Anadhani mimi nitakula wapi wakati ajira zenyewe wanapeana wakubwa?” alihoji mwanamke huyo huku akiondoka eneo hilo baada ya kutulizwa mizuka na wenzake.
