kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Tuesday 4 June 2013

MAELFU YA WATANZANIA WALIVYOJITOKEZA KUPOKEA MWILI WA ALBERT MANGWEHA AIRPORT....!!


Msanii Mchizi Mox akiwa mbele kabisa wakati
mwili umewasili uwanja wa ndege wa J.K NYERERE
AIRPORT....
Baadhi ya wasanii na waandishi wa habari wakiteta
 jambo wakati wakisubiri mwili....

Msanii Madee toka Tip Top Connection akihojiwa na
kituo kimoja cha Television uwanjani hapo...
Lamar Niekamp Producer wa Fishcrab kushoto na Proffesor J
walikuwepo kuupokea mwili wa
Ndugu yetu Albert Mangweha.....!!

Hapa Mwili ndio ulikuwa unatoka ndani ya uwanja wa ndege.....
Mwili ukiwa umekabidhiwa kwa wahusika tayari
kwa kuelekea Hospitali ya Taifa
Muhimbili....
Umati wa watu ulivyofurika kupokea mwili wa
ndugu yetu Albert Mangweha....

WAOMBOLEZAJI WASIMAMISHA GARI LILILOBEBA MWILI WA MAREHEMU NGWAIR WAKITAKA WAUBEBE MPAKA MUHIMBILI, TAZAMA PICHA HAPA


Muda huu ni msafara wakumpeleka marehemu Albert Mangweha hospitali kuu ya Mwimbili kumpumzisha. Hapa barabarani ni wananchi wamezuia gari lililobeba
jeneza na wakitaka litolewe nje walibebe mpaka hospital ya Mwimbili.

INTERVIEW YA KWANZA YA JOSE MOURINHO BAADA YA KURUDI RASMI CHELSEA

VIDEO & PHOTOS: NEYMAR ATAMBULISHWA NA KUONGEA NA MASHABIKI WA BARCELONA KWA MARA YA KWANZA @CAMP NOU


GARI JIPYA ALILONUNULIWA DIAMOND NA KAMPUNI YA COCACOLA. LICHEKI HAPA

Ukikutana na Diamond mtaani akiwa na mchuma mpya wenye rangi nyeusi, usishtuke sana, jua ni courtesy of Cocacola.
16859d0ccbab11e29f3f22000a1f978e_7
Inavyoonekana ni kuwa Cocaboy kama anavyojiita siku hizi, amenunuliwa gari jipya na wadhamini wake kampuni ya vichwaji ya Cocacola.
“Ya all ready know what it’s….. tukutane Fuel station!! #CocaCola Mumetishaaaaaa,” aliandika jana kwenye picha ya Instagram ya gari hilo likiwa na maganda yake.
“Chatin infront of my Small baby… on @channeloafrica interview at my clib,” aliongeza.
5df7e19acbb011e293af22000a9e05e8_7
Siku nzima ya juzi, hitmaker huyo wa Kesho alikuwa busy kwenye interview na kituo cha runinga cha Channel O.
af471706cb8211e2896422000a1fb003_7

MWANA FA NA JIDE KWA MARA NYINGINE WATAFANYA SHOW YAO SIKU MOJA, SOMA HAPA

Ikiwa ni siku chache baada ya wasanii kuahirisha show zao kufuatia kuondokewa mpendwa wetu Albert Mangwea, miongoni mwa show kubwa zilizoahirishwa ni ya Lady Jay Dee (Miaka 13 ya Lady JayDee) na ya Mwana FA (The Finest) zilizokuwa zifanyike siku moja (May 31),show hizi zinaweza kufanyika tena siku moja kwa kuwa wasanii hao wametaja tarehe inayofanana.


May 28 ambayo ndiyo siku aliyofariki Mangwea mwana FA alithibitisha kuahirisha show yake, lakini alipoulizwa siku ambayo anadhani atairudia show hiyo, yeye alifunguka kupitia akaunti yake ya twitter na kuitaja June 14.
 “Sina uhakika,but I'll pick June 14th kama brother tutakuwa tushampumzisha"@umykitwana”, alitweet Mwana FA a.k.a Binamu.
Kwa upande wake Lady Jay Dee ambae kwa sasa a.k.a yake mpya ‘Anaconda’ inaonekana ku-take over ametumia akaunti yake ya twitter kuiweka wazi tarehe ya show yake alipokua akijibu swali la fan wake ambae atasherehekea siku moja ya kuzaliwa na msanii huyo (June 15).
“@MteiHaikaJ Gud. Chukua hii tar 13 June Mahakamani, tar 14 June miaka 13 ya Jide na tar 15 June Bday ya Jide. Let's celebrate long week end.”Alitweet Lady Jay Dee June 2.
Kwa tweets za wakali hawa wa bongo fleva inaonesha kabisa kuwa show zao zinaweza kufanyika june 14 japo Mwana FA alisema hana uhakika, labda kama atatangaza siku nyingine tena. June 14,tunatarajia kuwa marehemu Ngwair atakuwa amekwisha pumzishwa kwenye nyumba yake ya milele huko Morogoro.
CHANZO : LEOTAINMENT

SAMAKI WA AJABU AVULIWA UNGUJA


NI AJABU NA INASTAJABISHA:
Mchangamle kizimkazi,walikusanyika na kumshanga samaki
huyu wa ajabu ambae wavuvi na wakazi
wa maeneo hayo hawakuwahi kumwona,maana samaki huyu
aelewiki ni CHUI,DUMA au ni nini....
Nikaona nisistajabike mwenyewe nikuweke hapa wewe mpitiaji
wa pincode presenter upate kujua
yanayoendelea Dunia.....kwangu mimi ni ajabu sijawahi
kuona kiumbe kama hicho.....

MAKALIO YAANIKWA MBELE YA WABUNGE KATIKA SHINDALO LA MISS TABORA


Mmoja wa washabiki wa muziki wa kizazi kipya ambaye alivaa vazi lililoacha  matako  nje....

Shabiki huyo  alipanda jukwaani kumkumbatia  msanii  maarufu nchini , Ommy Dimpoz  wakati alipokuwa akitoa burudani katika mashindano ya Redds Miss Tabora.

Tukio hilo la aibu lilitokea  mbele ya  wabunge....
Mbunge wa Jimbo la Sengerema  Bw.William Ngereja akiwa na Diwani wa kata ya Kitete manispaa ya Tabora Bw.Daniel Mhina ambaye alikuwa MC katika onesho hilo lililofanyika katika ukumbi wa Frankman Hotel mjini Tabora.
Ommy Dimpoz akitokwa na machozi wakati akitumbuiza jukwaani alipofikia hatua ya kumkumbuka marehemu msanii  maarufu Mangwea.
Ommy Dimpoz alionesha kukubalika zaidi katika onesho hilo
Mbunge Ngereja akiwa na mbunge wa vitimaalum mkoani Tabora wakijaribu kucheza kwa pamoja muziki uliokuwa ukiimbwa na Ommy Dimpoz.

Redds Miss Tabora 2013 Annastazia Donald(19)ambaye ni mwanafunzi wa Theofil Kisanji University,kushoto ni mshindi wa pili katika kinyang'anyiro hicho  Sabrina Juma(18) kutoka chuo cha African Utalii na mshindi wa tatu ni Cornecia Cossei(21)kutoka chuo cha Utumishi wa Umma Tabora.  

PUSH MOBILE YATOA MILIONI 10 KAMA MALIPO YA AWALI YA MAUZO YA NYIMBO ZA NGWEA, HILI NDO TAMKO WALILOTOA LEO

Baada ya watanzania wengi na wadau wa muziki kujiuliza kuhusu hatma ya malipo ya nyimbo za marehemu Albert Mangwea zilizokuwa zikitumika katika miiito ya simu, maswali hayo yamepatiwa majibu na kampuni ya Push inayohusika na zoezi zima la kuuza miito ya simu (CBRT).

Kampuni hiyo imetoa tamko rasmi na kuwahimiza watanzania na wapenzi wa Ngwea kuendelea kununua kwa wingi nyimbo zake kama miito ya simu kwa kuwa malipo yake yanaendelea kusimamiwa na Bongo Records ambao ndio wasambazaji wa kazi za Marehemu.

MWILI WA ALBERT MANGWEHA ULIVYOAGWA JANA NCHINI SOUTH AFRICA-tar 03.06.2013



Ngwair-SA
Mwili wa Marehemu Ngwair utawasili leo jijini Dar Es Salaam na kuagwa na fans, marafiki na ndugu katika viwanja vya leaders club, kinondoni kabla ya safari ya kwenda Morogoro, ambapo atazikwa huko karibu kabisa na kaburi la baba yake mzazi …
R.I.P Albert Mangweha.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiGZzkgoGcdDxp2EZsSM6I43LF-RUcCI-nVYxkrxF4eXeI24n33a3t_roOgUpirnl89vM48RREG42btFSsRTe4BRmNEJrsI4AfH3Jo3udLlKfBXgscx9x0cHiHqjqhw9Z17xOgXr1IQigwz/s640/IMG-20130603-WA006.jpg
Shughuli ya kuaga mwili  wa mangwea nchini South Africa.....