kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Wednesday 29 May 2013

MTANZANIA FEZA AZIDI KUNGA'ARA BIG BROTHER AFRICA....AUKWAA UKUU WA KAYA

Tunaenda vizuri, bahati inaonekana kutuangukia watanzania kwani mshiriki Feza jana ameukwaa ukuu wa kaya ama kwa lugha ya ki-big brother ‘Head of House’.

Ilikuwaje?

Baba mwenye nyumba, biggie, alitoa task ambayo washiriki walitakiwa kuelekea bustanini na kuchagua box, ambaye angechukua box la ushindi ndo huyo angekuwa mkuu wa kaya. Kama zali, bahati hiyo ilimuangika mrembo Feza. Washiriki wenzie akiwemo mtanzania Nando, walimkumbatia kwa furaha kama ishara ya kumpongeza.

Iko hivi, ukichaguliwa kuwa mkuu wa kaya, unauwezo wa kumuokoa mtu ambaye anakuwa amependekezwa atoke katika wiki hiyo. Usipofanya hivyo basi wewe mwenyewe unawekwa kikaangoni.

Feza alitumia nafasi hiyo kumuokoa Elikem ambaye ni mshiriki kutoka Ghana na kumuweka kikaangoni Betty kutoka Ethiopia. Hiyo ni siri ambayo Feza inabidi aitunze hadi siku ya Jumapili wakati wa Eviction.

Hii issue ya kumuokoa Elikem wa Ghana, je ni dalili ya shemeji shemeji mbona wazima taa? Endelea kufuatilia..

PICHA YA HOSPITALI(Helen Joseph),Ulipohifadhiwa Mwili wa Marehemu albert Mangwea



Ngwea amefariki dunia jana asubuhi katika moja ya vitongoji vya jiji la Johannesburg na baadaye wenzake walimkimbiza katika Hospitali ya St Helen Joseph.

RIBERY ALALA KITANDA KIMOJA NA KOMBE LA ULAYA PAMOJA NA MKEWE


Winga wa Bayern Munich Franck Ribery amefichua kwamba alilichukua kombe la ubingwa wa ulaya na kwenda kulala kufuatiwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Borrusia Dortmund.

Mabingwa wa Bundesliga wamefika kwenye fainali ya Champions League mara tatu katika mika minne lakini wameshinda ubingwa wa ulaya kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2001.


Na Ribery akazungumzia namna alivyosherehekea ubingwa huo mara baada ya mchezo: "Nilikuwa macho mpaka saa 11 au 12 asubuhi,"  Sky Sports News.

"Nilienda kulala kabla ya saa 12 na nikachukua kombe la ulaya nikaenda nalo kulala kwenye kitanda kimoja pamoja na mke wangu."

HII NDIO SABABU INAYODAIWA KUSABABISHA KIFO CHA NGWAIR. SOMA HAPA

ripoti kamili
Taarifa Nilizo Pata Kutoka South
Africa Kutoka Kwa Hussein
Original Ambaye Yupo Pretoria
Amesema Ngwear Amefariki Leo

Asubuhi. Alikuwa Ghetto Moja Na
Msanii M To The P.
Walivyokwenda Kuwagongea
Asubuhi Walikuta Ngwear
Amefariki Na M To The P
Amepoteza Fahamu Kabisa. Pia
Daktari Ameshatoa Taarifa Kwa
Watu Wa Karibu Wa Ngwear
Huko South Africa. Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.mtu wa karibu anasema walitakiwa kurudi dar leo lakini waliwakuta wamezima kwenye room wote wawili baada ya kuji overdose madawa ya kulevya na M to the P yupo hoi hospitali

KUTOKA KWA ROMARIO MPAKA RONALDINHO - JE NEYMAR ATAFUATA NYAYO ZA WABRAZIL WENZIE NA KUTAMBA CAMP NOU

Romário (1993), Ronaldo (1996), Rivaldo (1997), Ronaldinho (2003) na Neymar (2013). Neymar anajiunga ma urithi mzuri wa washambuliaji wa Brazil unaoundwa na wanaume wanne waliopata mafanikio makubwa katika miongo kadhaa iliyopita na kupata mafanikio makubwa ndani ya Nou Camp - sasa ni zamu  Neymar da Silva.

Romário na Ronaldo
Romário aliigusa mioyo ya mashabiki wa Barca kwenye msimu wa 1993-4, wakati alipopewa jina la “cartoon footballer” kutokana na kuwa uwezo mkubwa mno wa kucheza soka. Aliposajiliwa alihaidi kufunga mabao 30 ya ligi na akatimiza ahadi yake huku kikosi cha Cruyff kikishinda ubingwa msimu huo, Romario alirudi Brazil baada ya nusu ya msimu uliofuatia.

Mara baada ya Romario kuondoka kinda la miaka 19 - Ronaldo De Lima aliwasili Camp Nou. Alikuwa na nguvu, mwenye ujuzi na mwenye uchu wa mabao - kwenye msimu wake wa kwanza alifunga mabao 47 kwenye mechi 51.

Rivaldo na Ronaldinho
Wakati Ronaldo alipohamia Inter, Rivaldo akaja Camp Nou akitokea Deportivo. Rivaldo akawa nyota wa kikosi cha Van Gaal kilichoshinda ligi mara mbili. Alifanikiwa kushinda mchezaji wa dunia mwaka 1999.

Kuwasili kwa Ronaldinho mwaka 2003 kukaleta mageuzi makubwa kwa klabu ya Catalunya na kuleta tabasamu lilopotea na mashabiki wa Barca. Baada ya ukame wa miaka mitano bila kombe, aliiongoza Barca kushinda ubingwa wao wa pili wa ulaya jijini Paris na kushinda uchezaji bora wa ulaya na dunia kwa mara kadhaa. 

Evaristo, Giovanni and Anderson
Romário, Ronaldo, Ronaldinho na Rivaldo wanaweza kuwa ndio washambuliaji wa kibrazil waliopata mafanikio makubwa zaidi, lakini hawakuwa wabrazil pekee walioleta sura za furaha Camp Nou. Kwa mfano miaka ya1950s, Evaristo de Macedo alifunga mabao 173 kwenye 219. Miongo kadhaa baadae mwishoni mwa miaka ya 90, Giovanni Silva na Sony Anderson pia walileta sura za furaha Catalunya kwa viwango vyao.

Sasa ni zamu ya Neymar - je atafuata nyayo za magwiji ya Brazil waliomtangulia kucheza Camp Nou na kuwafunika kabisa kimafanikio? Muda utaongea.

E-Newz, 28 May 2013 ( WAKIZINGUMZIA KIFO CHA MANGWEAR )

DIAMOND AFANYA KUFURU TEMEKE, WATU WAZUNGUKA GARI LAKE ASINDIKIZWA NA GARI LA POLISI