kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Saturday 25 May 2013

HUU NDIO UCHAMBUZI NA UTABIRI WANGU WA FAINALI YA BORRUSIA DORTMUND VS BAYERN MUNICH

FC Bayern wanakutana na mtihani mgumu usiku wa leo watakapocheza dhidi ya Borussia Dortmund kwenye dimba la Wembley jijini London. Leo ni siku ya kuondokana na mkosi mkubwa unaowatawala mabavarians ambao ndio timu inayoongoza kwa kufungwa kwenye UEFA Champiosn League - leo ni siku ya kufuta machungu kwa kupoteza mechi ya fainali ya mwaka jana ambayo walistahili kushinda ingawa bahati haikuwa upande wao.
Hii ni fainali ya kwanza ya wajerumani ambao wanastahili kuwemo kwenye fainali hiyo. Utakuwa mchezo mzuri wa kukumbukwa.

Dortmund, klabu inayoibuka kuwa na nguvu barani ulaya

Majeruhi: Mario Götze
Baada ya kusemwa kuwa kutolewa kawenye hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa ulaya msimu wa 2011-12, Dortmund hatimaye wameyachukulia uamakini mashindano haya kwa gaharama ya kupoteza ubingwa wa nyumbani.
Ingawa, mchezo wao kwenye Champions League umekuwa wa aina yake. Nguvu, ushirikiano, mbinu za mchezo wao zimekuwa nzuri kiasi cha kuvishinda vilabu kama Real Madrid.
Mario Götze, kiungo mchezashaji wao, ataukosa mchezo huo kutokana na majeruhi ya misuli. Alijaribu kurudisha fitness yake kupitia mazoezi, lakini bahati haikuwa yake na akaawambia mchezo wake wa mwisho wa msimu huu ulikuwa pale Santiago Bernabeu. Ujuzi ambao BVB wataukosa ni pasi muhimu, kukimbiza mpira na mashuti yenye madhara
Wachezaji wa kuchungwa.
Kukosekana kwa Gotze kutamuacha mchezashaji Marco Reus. Kiungo huyo mshambuliaji anaweza kufanya runs za hatari pia kupiga mashuti na kutoa pasi za mwisho za hatari. Kazi ya kumzuia Reus kwa hakika atapewa kiungo mkabaji wa Bayern Javi Martinez ambaye aliweza kuwazima Iniesta na Andrea Pirlo kwenye mechi za raundi zilizopita.
Robert Lewandowski amegeuka kuwa mshambuliaji wa kiwango cha dunia, ameonyesha utulivu mbele ya lango la adui ambao washambuliaji wanakosa. Ana control nzuri ya mpira, anapiga mashuti yenye kulenga goli.
Muhimu zaidi, ni hazina ya Dortmund kwenye kulinda lango - golikipa Roman Weidenfeller. Uwezo wake wa kudaka uliinyima Bayern ushindi kwenye michezo kadhaa iliyopita msimu huu.
 Beki wa kati Mats Hummels anaweza akacheza mechi ya fainali pamoja na kuwa na majeruhi. Kitu cha kuvutia kuhusu yeye ni kwamba pamoja na mlinzi kwa ujumla, lakini pia anaweza akaigharimu timu yake kwa makosa ya kizembe.
Ilkay Gündogan ni kiungo mzuri mkabaji ambaye anaweza kufanya dribbling vizuri kuwapita mabeki wa Bayern, lakini sio mzuri kwa mipira ya juu ambao ndio silaha inayohitajika kuweza kuisimamisha Bayern.
Wakati uzuri wa Dortmund inacheza vizuri hata bila kuwa na mpira, mchezo mzuri wa kupasiana unaweza ukawadhuru kwenye nusu yao ya uwanja. Pia wana udhaifu mkubwa kwenye mipira mirefu.

Bayern, wanapaa kwenye muda muafaka

Majeruhi: Badstuber, Kroos.
 Huu ni mchezo unaomaanisha kila kitu kwa Bayern, ambayo ipo kwenye kiwango cha juu kwenye muda sahihi.
The bavarians wapo kwenye moto safari hii kwenye ulinzi na ushambuliaji. Udhaifu wao uliowagharimu msimu uliopita ni nguvu ya akili, udhaifu ambao umeshashughulikiwa. Sasa hivi wana ile hali ya winning mentallity - angalia namna walivyotoka nyuma na kuwafunga Borrusia Monchengladbach 4-3.
Franck Ribéry yupo kwenye kiwango cha dunia akicheza winga ya kushoto, unaweza ukasema hivyo pia kwa Thomas Muller ambaye anashughulika na majukumu ya kushambulia aliyokuwa nayo Toni Kroos.
Bastian Schweinsteiger na kila kitu cha kutoa kwenye mchezo huu. Ni package iliyokamilika kama mchezaji, box to box midle, yupo kwenye kiwango cha juu sana.
Uzuri wa Bayern hivi sasa mpaka wachezaji ambao walikuwa wavivu kama Arjen Robben wanakaba, timu yote inakaba kwa pamoja na wanashambulia kwa pamoja.

MBINU

Mtu yoyote ambaye angeniuliza timu gani yenye mbinu kali kati ya BVB na Real Madrid: jibu lingekuwa Dortmund. Sio tu kwamba wanaijua vizuri Bayern Munich, bali pia ni hatari sana kwenye mchezo wa kushambulia. Ubora wa umewaumiza wapinzaani wengi, lakini staili yao inayofanana na Barca ndio ambayo Bayern wanaiweza kwenye kucheza dhidi nayo.
Dortmund watahitaji kucheza mchezo wa kupelekea mashambulizi mbele, kupitia katikati ya uwanja kwa sababu ndio mchezo wanaouweza zaidi - wakipeleka mipira kwa Robert Lewandoski.
Kwa upande wa Bayern, mshambuliaji Mario Mandzukic (au Mario Gomez) wataungana na mchezeshaji Thomas Müller kuzuia mistari ya pasi kwenye kiungo kwa presha huku wakirudi nyuma taratibu
Hii itaaminisha Dortmund itabidi watumie zaidi winga kwenda mbele. Hivyo ikiwa BVB watapeleka mpira upande wa kushoto Arjen Robben na Javi Martinez wata press upande huo kuzia mashambulizi. Ikiwa watapeleka upande wa kushoto Frank Ribery na Bastian Schweinsteiger watazuia upande huo. Hii itawasaidia Lahm na Alaba kupambana akina Reus.
Hili linaweza kuwalazimisha BVB kutumia mipira ya juu ambayo Bayern wanaimudu pia, hivyo kuwafanya Dortmund kuwa na option moja tu kucheza sana mpira kwenye nusu yao ya uwanja na kujaribu kufanya counter. Hivyo nafasi zao za kufunga zitakuwa pungufu - au italawazimu wachezaji wa Dortmund kuwashinda wa Bayern kwenye vita ya one-on-one au kunufaika na makosa ya wachezaji wa Bayern kama ilivyokuwa kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Monchengladbach wiki iliyopita. Lakini pia Bayrn wanaweza wakawa wamepata funzo kupitia mchezo huo na kutoruhusu makosa yale yasijirudie dhidi ya Borrusia Dortmund usiku wa leo pale Wembley.
Ikiwa Bayern watacheza kwenye kiwango cha juu usiku wa leo basi itawachukua BVB kutumia vipaji binafsi zaidi vya wachezaji kuweza kushinda.
 
Vita binafsi leo hii itakuwa kati ya winga wa kushoto wa Bayern Frank Ribery vs Lukasz Piszczek. Kwa spidi aliyonayo Mpoland huyo, na uwezo wake wa kuzuia itamchukua uwezo mwingi sana Frank Ribery kuweza kupita.
Mara ya mwisho Bayern wameifunga Dortmund, walimtumia zaidi Toni Kroos na uwezo wake wa kumiliki mpira - Muller hana uwezo mkubwa wa kukaa na mpira kama ilivyo kwa Kroos hivyo mambo yanaweza magumu kiasi.

Utabiri wangu nawapa Bayern nafasi ya kushinda. Mafunzo waliyoyapata miaka iliyopita hasa msimu uliopita dhidi ya Chelsea yatawapa hali ya kupigana zaidi. Hata kama wataanza kufungwa, watashindana na kuhakikisha safari hii wanaepukana na mkosi wa fainali ya Champions League. Dortmund wana mtindo wa kupaniki - angalia katika mechi ya pili dhidi ya Madrid nusura waondolewe pamoja kuwa walikuwa na hazina ya mabao 4-0.

Vikosi vinavyoweza kuanza

FC Bayern (4-2-3-1) Neuer – Lahm, Boateng, Dante, Alaba – Martinez, Schweinsteiger – Robben, Müller, Ribéry – Mandzukic
Borussia Dortmund (4-2-3-1) Weidenfeller – Piszczek, Subotic, Hummels, Schmelzer – Gündogan, Kehl – Blaszczykowski, Reus, Grosskreutz – Lewandowski
Location: Wembley Stadium, London
Referee: Nicola Rizzoli (Italy)

MWAMUZI WA AFRIKA KUSINI KUICHEZESHA STARS MOROCCO


Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).
Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.
Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.
Kamishna wa mechi hiyo ni Robert Mangollo-M’voulou wa Gabon wakati mtathimini wa waamuzi (referee assessor) ni Charles Masembe kutoka Uganda.
Taifa Stars ambayo iko chini ya Kocha Kim Poulsen, na ikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari iko kambini katika hoteli ya Tansoma ikiendelea kujinoa kwa ajili ya mechi hiyo ambapo kabla itajipima na Sudan (Nile Crocodiles) Juni 2 mwaka huu jijini Addis Ababa, Ethiopia.
Ratiba ya mazoezi kwa timu hiyo ni kama ifuatavyo;
Mei 22                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni   Uwanja wa Karume
Mei 23                 Saa 10 jioni                             Uwanja wa Karume
Mei 25                 Saa 1 asubuhi na Saa 10 jioni     Uwanja wa Karume
Mei 26                 Saa 3 asubuhi                            Uwanja wa Karume

AMRI KIEMBA ASAINI YANGA

WAKATI Haruna Niyonziam akiwa amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga, habari zilizotufikia hivi punde zinasema kiungo wa Simba, Amri Kiemba amesajiliwa na Yanga tayari kwa kuitumikia timu hiyo kwa msimu ujao.
Akizungumza na mtandao huu, mtu mmoja kutoka kamati ya usajili ya Yanga, amesema Kiemba amesajiliwa kwa mkataba wa miaka miwili ili kuongoza nguvu katika safu ya usajili ya Yanga.
Mtandao huu unaahidi kuwasiliana na Kiemba muda mfupi atakapotoka mazoezini katika kambi ya Taifa Stars kujiandaa na mechi ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2014.
Atakapotoka mazoezini mtandao huu utawasiliana naye kiungo huyo ili aweze kueleza ukweli juu ya usajili wake kwa Yanga.
Kiemba aliwahi kuichezea Yanga miaka ya nyuma kabla ya kutimka katika timu hiyo.

BREAKING NEWS: RAMA MLA WATU AACHIWA HURU




Mahakama kuu kanda ya Dar es Salaam imeamua kumuachia huru Ramadhani Selemani Mussa ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya kukutwa na kichwa cha mtu. Rama, ambaye muda wote huo alikuwa rumande gereza la Segerea akisota kusubiri hukumu yake, alikamatwa hospitali ya Muhimbili mwaka 2008 ambapo pia alikiri kuwa alikuwa na tabia ya kula nyama za watu ambayo amefundishwa kichawi toka alipokuwa mdogo. Mahakama imemuachia huru kwasababu mtuhumiwa alitenda kosa hilo pasipo kuwa na akili timamu. Hata hivyo mahakama hiyo imetoa agizo la kuendelea kumuweka kijana huyo katika hospitali ya wagonjwa wenye matatizo ya akili, hospitali ya Isanga iliyopo Dodoma mpaka pale atakapona ndipo aruhusiwe kurudi mtaaani.habari kutoka karibu ndani

KANYE WEST AFUNGUKA RASMI....ATEGEMEA KUWA BABA HIVI KARIBUNI.....

BIG BROTHER AFRICA(THE CHASE) NDANI YA KING'AMUZI CHAKO J2 HII

DIAMOND,NEY WA MITEGO BAADA YA KUANGUSHA SHOO YA KIJANJA DAR LIVE HAWA HAPA TENA MAISHA CLUB J2 HII

THIS IS DIAMOND-IN CONGO