kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Saturday 25 May 2013

HUU NDIO UCHAMBUZI NA UTABIRI WANGU WA FAINALI YA BORRUSIA DORTMUND VS BAYERN MUNICH

FC Bayern wanakutana na mtihani mgumu usiku wa leo watakapocheza dhidi ya Borussia Dortmund kwenye dimba la Wembley jijini London. Leo ni siku ya kuondokana na mkosi mkubwa unaowatawala mabavarians ambao ndio timu inayoongoza kwa kufungwa kwenye UEFA Champiosn League - leo ni siku ya kufuta machungu kwa kupoteza mechi ya fainali ya mwaka jana ambayo walistahili kushinda ingawa bahati haikuwa upande wao.
Hii ni fainali ya kwanza ya wajerumani ambao wanastahili kuwemo kwenye fainali hiyo. Utakuwa mchezo mzuri wa kukumbukwa.

Dortmund, klabu inayoibuka kuwa na nguvu barani ulaya

Majeruhi: Mario Götze
Baada ya kusemwa kuwa kutolewa kawenye hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa ulaya msimu wa 2011-12, Dortmund hatimaye wameyachukulia uamakini mashindano haya kwa gaharama ya kupoteza ubingwa wa nyumbani.
Ingawa, mchezo wao kwenye Champions League umekuwa wa aina yake. Nguvu, ushirikiano, mbinu za mchezo wao zimekuwa nzuri kiasi cha kuvishinda vilabu kama Real Madrid.
Mario Götze, kiungo mchezashaji wao, ataukosa mchezo huo kutokana na majeruhi ya misuli. Alijaribu kurudisha fitness yake kupitia mazoezi, lakini bahati haikuwa yake na akaawambia mchezo wake wa mwisho wa msimu huu ulikuwa pale Santiago Bernabeu. Ujuzi ambao BVB wataukosa ni pasi muhimu, kukimbiza mpira na mashuti yenye madhara
Wachezaji wa kuchungwa.
Kukosekana kwa Gotze kutamuacha mchezashaji Marco Reus. Kiungo huyo mshambuliaji anaweza kufanya runs za hatari pia kupiga mashuti na kutoa pasi za mwisho za hatari. Kazi ya kumzuia Reus kwa hakika atapewa kiungo mkabaji wa Bayern Javi Martinez ambaye aliweza kuwazima Iniesta na Andrea Pirlo kwenye mechi za raundi zilizopita.
Robert Lewandowski amegeuka kuwa mshambuliaji wa kiwango cha dunia, ameonyesha utulivu mbele ya lango la adui ambao washambuliaji wanakosa. Ana control nzuri ya mpira, anapiga mashuti yenye kulenga goli.
Muhimu zaidi, ni hazina ya Dortmund kwenye kulinda lango - golikipa Roman Weidenfeller. Uwezo wake wa kudaka uliinyima Bayern ushindi kwenye michezo kadhaa iliyopita msimu huu.
 Beki wa kati Mats Hummels anaweza akacheza mechi ya fainali pamoja na kuwa na majeruhi. Kitu cha kuvutia kuhusu yeye ni kwamba pamoja na mlinzi kwa ujumla, lakini pia anaweza akaigharimu timu yake kwa makosa ya kizembe.
Ilkay Gündogan ni kiungo mzuri mkabaji ambaye anaweza kufanya dribbling vizuri kuwapita mabeki wa Bayern, lakini sio mzuri kwa mipira ya juu ambao ndio silaha inayohitajika kuweza kuisimamisha Bayern.
Wakati uzuri wa Dortmund inacheza vizuri hata bila kuwa na mpira, mchezo mzuri wa kupasiana unaweza ukawadhuru kwenye nusu yao ya uwanja. Pia wana udhaifu mkubwa kwenye mipira mirefu.

Bayern, wanapaa kwenye muda muafaka

Majeruhi: Badstuber, Kroos.
 Huu ni mchezo unaomaanisha kila kitu kwa Bayern, ambayo ipo kwenye kiwango cha juu kwenye muda sahihi.
The bavarians wapo kwenye moto safari hii kwenye ulinzi na ushambuliaji. Udhaifu wao uliowagharimu msimu uliopita ni nguvu ya akili, udhaifu ambao umeshashughulikiwa. Sasa hivi wana ile hali ya winning mentallity - angalia namna walivyotoka nyuma na kuwafunga Borrusia Monchengladbach 4-3.
Franck Ribéry yupo kwenye kiwango cha dunia akicheza winga ya kushoto, unaweza ukasema hivyo pia kwa Thomas Muller ambaye anashughulika na majukumu ya kushambulia aliyokuwa nayo Toni Kroos.
Bastian Schweinsteiger na kila kitu cha kutoa kwenye mchezo huu. Ni package iliyokamilika kama mchezaji, box to box midle, yupo kwenye kiwango cha juu sana.
Uzuri wa Bayern hivi sasa mpaka wachezaji ambao walikuwa wavivu kama Arjen Robben wanakaba, timu yote inakaba kwa pamoja na wanashambulia kwa pamoja.

MBINU

Mtu yoyote ambaye angeniuliza timu gani yenye mbinu kali kati ya BVB na Real Madrid: jibu lingekuwa Dortmund. Sio tu kwamba wanaijua vizuri Bayern Munich, bali pia ni hatari sana kwenye mchezo wa kushambulia. Ubora wa umewaumiza wapinzaani wengi, lakini staili yao inayofanana na Barca ndio ambayo Bayern wanaiweza kwenye kucheza dhidi nayo.
Dortmund watahitaji kucheza mchezo wa kupelekea mashambulizi mbele, kupitia katikati ya uwanja kwa sababu ndio mchezo wanaouweza zaidi - wakipeleka mipira kwa Robert Lewandoski.
Kwa upande wa Bayern, mshambuliaji Mario Mandzukic (au Mario Gomez) wataungana na mchezeshaji Thomas Müller kuzuia mistari ya pasi kwenye kiungo kwa presha huku wakirudi nyuma taratibu
Hii itaaminisha Dortmund itabidi watumie zaidi winga kwenda mbele. Hivyo ikiwa BVB watapeleka mpira upande wa kushoto Arjen Robben na Javi Martinez wata press upande huo kuzia mashambulizi. Ikiwa watapeleka upande wa kushoto Frank Ribery na Bastian Schweinsteiger watazuia upande huo. Hii itawasaidia Lahm na Alaba kupambana akina Reus.
Hili linaweza kuwalazimisha BVB kutumia mipira ya juu ambayo Bayern wanaimudu pia, hivyo kuwafanya Dortmund kuwa na option moja tu kucheza sana mpira kwenye nusu yao ya uwanja na kujaribu kufanya counter. Hivyo nafasi zao za kufunga zitakuwa pungufu - au italawazimu wachezaji wa Dortmund kuwashinda wa Bayern kwenye vita ya one-on-one au kunufaika na makosa ya wachezaji wa Bayern kama ilivyokuwa kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Monchengladbach wiki iliyopita. Lakini pia Bayrn wanaweza wakawa wamepata funzo kupitia mchezo huo na kutoruhusu makosa yale yasijirudie dhidi ya Borrusia Dortmund usiku wa leo pale Wembley.
Ikiwa Bayern watacheza kwenye kiwango cha juu usiku wa leo basi itawachukua BVB kutumia vipaji binafsi zaidi vya wachezaji kuweza kushinda.
 
Vita binafsi leo hii itakuwa kati ya winga wa kushoto wa Bayern Frank Ribery vs Lukasz Piszczek. Kwa spidi aliyonayo Mpoland huyo, na uwezo wake wa kuzuia itamchukua uwezo mwingi sana Frank Ribery kuweza kupita.
Mara ya mwisho Bayern wameifunga Dortmund, walimtumia zaidi Toni Kroos na uwezo wake wa kumiliki mpira - Muller hana uwezo mkubwa wa kukaa na mpira kama ilivyo kwa Kroos hivyo mambo yanaweza magumu kiasi.

Utabiri wangu nawapa Bayern nafasi ya kushinda. Mafunzo waliyoyapata miaka iliyopita hasa msimu uliopita dhidi ya Chelsea yatawapa hali ya kupigana zaidi. Hata kama wataanza kufungwa, watashindana na kuhakikisha safari hii wanaepukana na mkosi wa fainali ya Champions League. Dortmund wana mtindo wa kupaniki - angalia katika mechi ya pili dhidi ya Madrid nusura waondolewe pamoja kuwa walikuwa na hazina ya mabao 4-0.

Vikosi vinavyoweza kuanza

FC Bayern (4-2-3-1) Neuer – Lahm, Boateng, Dante, Alaba – Martinez, Schweinsteiger – Robben, Müller, Ribéry – Mandzukic
Borussia Dortmund (4-2-3-1) Weidenfeller – Piszczek, Subotic, Hummels, Schmelzer – Gündogan, Kehl – Blaszczykowski, Reus, Grosskreutz – Lewandowski
Location: Wembley Stadium, London
Referee: Nicola Rizzoli (Italy)