kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Wednesday 23 April 2014

Hiki ndio kiasi cha fedha alicholipwa David Moyes baada ya kutimuliwa

article-2609490-1D411CD200000578-628_634x505Siku moja baada ya kutimuliwa kutoka kwenye kibarua cha kuifundisha klabu ya Manchester United imefahamika kwamba kocha David Moyes atalipwa fidia kutokana na klabu hiyo kuvunja mkataba wa miaka sita walioingia mwaka jana mwezi wa tano.
David Moyes atalipwa fidia ya £5million baada ya kufukuzwa kazi na Manchester United – ikiwa ni kipengele cha makubaliano ya mkataba wake na klabu hiyo.
Katika mkataba wa Moyes na United kulikuwa na kipengele kinachoeleza ikiwa Manchester United ingefeli kufuzu kucheza Champions League msimu huu basi ikatokea United wakaamua kusitisha mkataba wake basi fidia isingezidi mshahara wake wa miezi 12 ambao ni £5million.

No comments: