kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Friday 7 June 2013

KHADIJA KOPA KAFIWA NA MUMEWE, MWENYEWE AKIWA KWENYE MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIAN MKOANI RUKWA

Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa
 Rukwa na Mpanda
 wakimsindikiza kupanda ndege
 msanii wa taarab na malkia wa mipasho Tanzania
 Khadija Omar kopa kwenye uwanja wa
 ndege wa mpanda baada ya
 kupewa taarifa ya kufiwa 
na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leo alfajiri
 kutokana na ugonjwa, Bi Khadija
 Kopa alikua akitokea kwenye Maadhimisho ya
 siku ya Mazingira Duniani kitaifa
 yaliyoadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya (kushoto)
 akimfariji msanii wa taarab na malkia wa mipasho 
Tanzania,Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba
 maalum cha kupumzikia wageni kwenye
 uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya
kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki
 Dunia leo
 Bi Khadija Kopa alikua kwenye maadhimisho ya
 siku ya mazingira Duniani kitaifa 
yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa juzi.