kaa tayari kwa blog yangu mpya ya fashion JACK255.BLOGSPOT.COM....

SEARCH FOR ANYTHING IN THIS BLOG

Thursday 3 October 2013

Licha ya kuvuja kwenye internet, album ya Drake imeshika namba moja kwenye chart ya Billbord Top 200


drake-happy-sad-new-650

Licha ya kuvuja kwenye mtandao wiki moja kabla ya tarehe rasmi ya kutoka, album ya Drake Nothing wa The Same imeshika namba moja kwenye wiki yake ya kwanza tangu itoke na imekua album ya pili kwa kufanya mauzo mazuri kwa album zote zilizotoka kwenye wiki hii. Mafanikio mengine ambayo album ya “Nothing was the same” imepata ni kuyapita mauzo ya album za zamani kutoka kwa Drake.
Ndani ya wiki ya kwanza album yake ya “Take Care,” iliuza nakala 631,000, “Thank Me Later,”iliuza 447,000 , “So Far Gone,” iliuza nakala 73,000. Nothing was the same imeuza nakala  658,000 katika wiki ya kwanza na kuvunja rekodi ya album zake zilizopita.
Drake alifanyiwa interview na ex-girlfriend kwenye show ya 106&Park ikiwa ni moja ya promotion za album yake mopya. Drake alikuwa na mahusiano na binti huyu enzi hizo wakiwa Canada na hivi sasa ni mtangazaji mpya kwenye show hii ya BET

No comments: